Jumatatu, 20 Juni 2016

ushuhuda wangu baada ya kumpa Yesu Maisha yangu na AL Haj Meja Hasan





USHUHUDA WANGU ALHAJI MEJA HASAN

HISTORIA
Mimi Nilizaliwa mnamo mwaka 1990 katika kijiji cha Msowero, wilaya ya Kilosa, mkoa wa Morogoro.

Mnamo ALHAJI MEJA HASAN mwaka 1996 nilihamia Zanzibar na kuishi huko na kujiunga na dini ya Kiisilamu na kupata elimu ya msingi mnamo mwaka 1997 hadi mwaka 2003. Nilihitimu kidato cha nne mwaka 2007 nikiwa hukohuko Unguja.


Baada ya hapo nilijiunga na kikosi cha KZ cha ulinzi na usalama Zanzibar mwaka 2009 hadi 2010 May ndipo nilihitimu.


Baada ya hapo nilisoma masomo ya Kiitaliano na Kiingereza kwa mudawa  miezi 9.

Niliajiriwa katika Bank ya NCCT Zanzibar ambayo inabadilisha fedha za kigeni za kimataifa.

Nilianza kazi 2011 hadi 2015 ambapo mkataba wangu wa kufanya kazi miaka 10 ulikwisha.


  1. KABLA YA KUOKOKA

Nilipitia mambo magumu katika maisha yangu ambayo yalinusuru/ gharimu/ hatarisha maisha yangu.

Siku moja kuna wageni walitoka Mataifa mbalimbali duniani, na kati ya hao wageni mmoja anasadikika kwamba inaweza ikawa alitega bomu karibu na Bank.
 Sisi kama maaskari hatukujua lolote. Wakati tunalinda nilisikia sauti ya Mungu ikisema nami kwamba niondoke mahali hapo na kusogea mbali kidogo, bila kujua sababu niliitii ile sauti na ndipo bomu lilipolipuka na kuwalipukia wenzangu watatu na kupoteza maisha yao na mimi kunusurika.

Baada ya siku sita kupita niliacha kazi mnamo tarehe 07/11/2015 kabla hata ya mkataba wangu kuisha ambapo pia ilinigharimu kwa kampuni.


Kabla ya kuokoka nilidumu duniani kwa vile nilikuwa na pesa ambazo hazikunisaidia baadaye.


Siku mija niliota ndoto na nikaoneshwa huku kuna maji na huku kuna moto. Nikaambiwa na Malaika chagua unakotaka, nikabaki lalia niende wapi! Ndoto hiyo moja ilijirudia  kwa muda wa siku sita na ndipo nikachukua jukumu la kuacha kazi.


Nikaona hela sio bora japo ni bora, nikaamua kumfuata Mungu. Maisha yangu nilikula mirungi, nilivuta bangi na kunywa kila aina ya kilevi ili niwe fiti katika kazi yangu ambayo ilinilazimu.


  1. HATUA ZA KUOKOKA NA KUMFUATA BWANA NA MWOKOZI YESU KRISTO

Baada ya kuacha kazi nilimtafuta Mchungaji wa kiroho wa kanisa la Kipentekoste ambaye Mungu alisema nami, baada ya mafundisho mengi ya neno la Mungu alinitubisha sala ya toba na kuwa mkristo mwaminifu wa kanisa la Kipentekoste mwanzoni mwa mwezi Desemba 2015. Kupitia huyo mchungaji ikawa ni ukombozi mkubwa kwangu na mwanzo wa maisha mapya ndani ya wokovu.

Hadi leo tarehe 07/01/2016 ninaendelea na Yesu wangu vizuri na siku ya Jumapili wiki hii tarehe 10/01/2016 nitabatizwa ubatizo wa Yesu Kristo wa maji mengi ili kutimiliza au kutimiza haki yote. Kwa kupata zaidi mafundisho ya ubatizo fungua kwa biblianenohai@gmail.com  au click/ bofya hapo mbele UBATIZO WA MAJI MENGI.
Nilikuwa mwislamu tangu mwaka 1999 hadi mwaka 2015. Nimetumikia uislamu kwa muda wa miaka 16. Kwa muda wote niliotumikia uislamu nilikuja kugundua nilipotea na kuamua kumpa Yesu Kristo maisha yangu awe Bwana na Mwokozi wa maisha yangu.
Kwa sasa naishi maisha ya amani ndani ya Kristo Yesu Bwana na Mwokozi wa maisha yangu.
Bila kokoka na kumpa Yesu maisha yako Mbinguni hutakwenda wewe ndugu yangu ambaye bado haujaokoka. Yesu alikufa na kufufuka na sas yupo hai. Wengine wote walikufa na mifupa yao ipo kaburini hadi leo. Asanteni.

Jina langu niliitwa Alhakim Meja Hasan. Na kitambulisho changu cha kazi ni ID.EL/GUARD/no: Z.11036, Mwewe Security Company Ltd, PO Box 1203, Zanzibar, Mobile +255 777 421159/ 0786111957, Email mwewesc@gmail.com , position: Security Guard.
 
Kama unataka kuwasiliana nami tuwasiliane kwa Email hii njiayawokovu@gmail.com

NINGEPENDA VIJANA WENZANGU WA KI-AFRIKA NA TANZANIA MUWEZE KUSOMA USHUHUDA WANGU, MAANA NI USHUHUDA MKUBWA WA KUMTUMIKIA MUNGU KULIKO KUTUMIKIA PESA.


Ukimtumikia Mungu siku za maisha yako zitaongezwa kwa vile ni mpango wa Mungu. Ee ndugu yangu, Rafiki, jamaa na Mtanzania mwenzangu badilika kupitia ushuhuda wangu ulio na mapito makubwa sana.

(JESUS IS MY SAVIOUR/ YESU KRISTO NI MWOKOZI WANGU)
Baada ya kuokoka nampenda Mungu sana, kwa sababu ameniponya kutoka mautini.Ewe kijana mwenzangu chukua uamuzi sasa  wa kuokokoa yaani kuongozwa sala ya toba na kubatizwa maji mengi. Jina lako litafutwa katika kitabu cha hukumu na kuandikwa katika kitabu cha uzima wa milele.

Kama hujaokoka jina lako lipo katika kitabu cha hukumu na siku mija utaja kulia sana utakapokwenda katika moto wa milele, huko utajalia na kusaga meno


Badilikeni kupitia ushuhuda wangu. Soma Matendo 4:1-3. Yesu ni njia ya uzima (Jesus is way of life)
Jifunze kupitia maono yangu na chukua hatua ya kubadilika ili ili upate kuokolewa ewe Baba, mama, dada, kaka na ndugu yangu, bibi na babu yangu. Utapata uponyaji wa kiroho na kimwili, kuokoka na kubatizwa kwa maji mengi au maji tele.

Baada ya hapo utapata mahusiano mazuri na Mungu na kila jambo utakaloliomba litatimia au kutimizwa.
Ewe ndugu yangu usidanganyike na ubatizo wa maji kidogo hatakusaidia. Kubatizwa maana yake ni kuzikwa utu wa kale. Ubatizo wa maji kidogo maana yake umezika kichwa tu na kiwilili chako kipo nje kwa shetani.
Epukeni madhara ya uongo tafuteni kanisa la kiroho.


Makanisa yapo mengi TAG, FPCT, EAG(T), PENTEKOSTE NK na utapata thawabu.

Kwa mungu ilitangazwa manabii wengi watakuja kwa jina langu, hivyo tuwe makini sana.
Yesu alibatizwa ubatizo wa maji tele katika mto wa jordani. Ubatizo wa maji mengi maana yake unakufa pamoja na Kristo Yesu na unafufuka pamoja naye kwenye uzima wa milele.
Asante Mungu kwa uwepo wako na kunisaidia kutoa ushuhuda wangu na kuushuhudia kwa mataifa. Neno lako linapita kila neno.

Neno la Mungu likuinue kiroho na kukubariki.

Mungu ubariki ushuhuda wangu huu na ukutumikie siku zote kwa wote watakaousoma wabarikiwe na kubadili maisha yao milele na hata milele Amina.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni